
Timu ya Singida United imerejea kwenye ligi msimu huu baada ya kusota bondeni kwa muda mrefu, lakini wamerejea kwa kishindo kwa kuwa ni miongoni mwa vilabu ambavyo mfuko wao wa salio umetuna kutokana na pesa za wadhamini.
Singida wana wadhamini rasmi watatu (YARA, SportPesa na Puma) wana wadau pia wanaowawezesha kama NMB Bank, DTB Bank na Oryx wote hao wanaingiza mtonyo...