Mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu Tanzania bara 2016/17 ambao ulifanyika katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam ulipigwa mchezo wa Ngao ya Hisani kati ya Mabingwa wa Ligi Kuu msimu wa 2015/2016 Young Africans na mshindi wa pili wa Ligi Kuu Azam FC hiyo ikiwa ishara ya kukaribia kuanza kwa msimu mpya wa Ligi.
Mabingwa wa watetezi wa ligi kuu Tanzania bara timu ya Yanga SC imenyang’anywa Ngao ya Jamii na Azam FC baada ya kufungwa kwa mikwaju ya penati 4-1 baada ya timu hizo kutoka sare ya kufungana bao 2-2 katika mchezo huo.
Mshambuliaji Donald Ngoma alikuwa wa kwanza kupata goli la kwa mkwaju wa penati na dakika 2 baadae kuongeza goli la pili kwa kutumia vyema pasi ya Amissi Tambwe, Dakika ya 74 Shomari Kapombe aliipatia Azam bao la kwanza akitumia makosa ya mabeki wa Yanga John Bocco ‘Adebayor’ aliisawazishia Azam kwa mkwaju wa penati dakika ya 90 penati iliyotokana na beki wa Yanga kuushika mpira kwenye box.
0 comments:
Post a Comment