Raia wawili wa China, Ma Jun na Huifang Ma leo wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kujibu mashtaka mawili likiwamo la kushindwa kutumia Mashine ya Kodi za Kielektroniki (EFDs) katika biashara zao.
Jun na Ma, ambao wote ni wafanyabiashara na wakazi wa Mtaa wa Narung’ombe eneo la Kariakoo wanakabiliwa na kushindwa kutumia mashine za EFDs pamoja na kushindwa kujisajili katika kodi ya ongezeko la Thamani(Vat) wakati wakijua kufanya hivyo kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.
Hata hivyo, mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Jun hakuwepo mahakamani hapo kwa madai kuwa yupo nje ya nchi na upande wa mashtaka umeiomba Mahakama kutoa hati kwa ajili ya kumkamata mshtakiwa huyo.
Akisoma hati ya mashtaka, mbele ya Hakimu Mkazi Mwanadamizi Mfawidhi wa mahakama hiyo Said Mkasiwa, Wakili kutoka Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), Cherubin Chuwa alidai kuwa washtakiwa kwa pamoja walitenda makossa hayo Machi 23,mwaka huu.
Chuwa alidai siku hiyo ya tukio, washtakiwa hao ambao wanamiliki Kampuni ya HM Textile Co Ltd Iliyopo block 54 katika kiwanja namba 6 kilichopo mtaa wa Agrey eneo la Kariakoo, walishindwa kutumia mashine za EFDs kwa ajili ya kutoa risiti kwa wateja wao ambao walikuwa wanafanya manunuzi mbalimbali katika duka hilo ambalo linauza mapazia na nguo mbalimbali, huku wakijua kuwa ni kosa kisheria.
Mwandesha Mashtaka huyo aliendelea kudai kuwa, katika shitaka la pili ambalo pia linawakabili washtakiwa wote, inadaiwa kuwa muda na siku hiyo hiyo katika duka hilo, washtakiwa walishindwa kujisajili katika kodi ya ongezeko la Thamani(Vat) wakati wakijua kufanya hivyo kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.
Chuwa alidai washtakiwa hao walishindwa kujisajili katika Kodi ya Ongezeko la Thamani(Vat) ambayo ni kinyume cha sheria , na kwamba mashtaka hayo yamefunguliwa kupitia sheria za TRA.
Hata hivyo mshtakiwa wa pili, Huifang alikiri shtaka la kwanza huku shtaka la pili akikana kuhusika.
Kutokana na hatua hiyo wakili Chuwa alisema dhamana ya mshtakiwa huyo iko wazi ambayo ni kuwa na wadhamini wawili kila kutoka taasisi inayotambuliwa kisheria watasaini bondi ya Sh 3milioni na kuwasilisha mahakamani hati yake ya kusafiria.
Mshtakiwa huyo alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande hadi April 21, mwaka huu.
Latest News
Loading...
Wachina kizimbani kwa kukwepa kulipa kodi
Related Posts:
Msajili wa vyama vya siasa nchini atoa ya moyoni juu ya CHADEMA Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, amekionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuhusu mikutano ya hadhara na maandamano yanayotarajia kuanza Septemba 1 mwaka huu. Alhamis hii, Mwenyekiti wa… Read More
Salam za Wema Sepetu kwa mtoto wa Diamond Platnumz ‘Tiffah’ Msanii wa filamu Wema Sepetu anaendelea kuuthibitishia umma kwamba hana tena kinyongo na Ex wake wa zamani Diamond Platnumz baada ya Jumamosi hii kumwandikia ujumbe mzuri bintiye Diamond, Tiffah katika siku yake ya k… Read More
Kijana mbaroni kwa kumtukana Rais Magufuli hadharani Mgomo wa daladala Jijini Mwanza umesababisha kijana mmoja Jijini humo kutamka lugha chafu ndani ya gari ambayo alipewa lifti limemsababishia kuishia mikononi kwa sheria.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi akiz… Read More
Mgeja Atoa yamoyoni Juu ya Rais Magufuli ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, amesema hatua ya Rais John Magufuli kuzuia kufanyika kwa mikutano ya kisiasa nchini, imelenga kuminya demokrasia na serikali kutaka k… Read More
Mkuu wa Mkoa wa DSM Paul Makonda Apiga Marufuku Maandamano ya UKUTA, Awapa Rungu FFU Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda ameliagiza jeshi la polisi mkoa wa Dar es salaam kuhakikisha kwamba sheria zinafuatwa na kusiwepo kitu kinaitwa UKUTA ili wananchi waendelee na kazi zao kama kawaida.Akizungumza n… Read More
0 comments:
Post a Comment