Latest News
Loading...

VIDEO: Gari lililozama Baharini Kivukoni Dar es salam April 20 2016

April 20 2016 gari aina ya Toyota Hiace lililokuwa ndani ya Pantoni kuelekea Kigamboni Dar es salaam liliserereka na kuzama baharini ambapo inasadikiwa lilikuwa na watu wawili, uokoaji ulifanyika ambapo asubuhi jeshi la zimamoto na uokoaji lilifanikiwa kuupata mwili mmoja na mchana mwili wa pili wa Nice Karago ukapatikana... Source:Ayo...

Nyota ya Mbwana Samata Yazidi Kung'aa Baada ya Ushindi Mwingine Mnono wa Timu yake...

Usiku wa April 20 2016 kocha wa KRC Genk Peter Maes kaendelea kumuamini na kumpa nafasi ya kuanza katika first eleven yake nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania anayeichezea klabu hiyo Mbwana Samatta, Maes amempa nafasi Samatta ya kuanza mchezo wa pili mfululizo.Licha ya kuwa KRC Genk walikuwa nyumbani katika uwanja wao wa Cristal Arena kukabiliana na vinara wa Ligi hiyo...

TUCTA Yapinga Mpango wa Rais Magufuli Kukata Mishahara ya Watumishi wa Umma Kutoka Milioni 40 hadi 15 Kwa Mwezi

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (Tucta) limepinga mpango wa Rais John Magufuli wa kukata malipo ya mishahara ya watumishi wa umma kutoka Sh40 milioni kwa mwezi hadi Sh15 milioni. Akizungumza na viongozi wa vyama vya wafanyakazi Kanda ya Ziwa jijini Mwanza jana, Naibu Katibu Mkuu wa Tucta, Hezron Kaaya alisema uamuzi huo ni kinyume na sheria na utaligharimu...

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla Aonja Moto wa UKAWA.....Madiwani 34 Wakiongozwa na Meya wao Wasusia Kikao chake cha Kujitambulisha

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amekumbana na joto la Mbeya baada ya meya wa jiji hilo, Mchungaji David Mwashilindi na madiwani wake 34 kususia kikao chake cha kujitambulisha kwa wananchi, baada ya kudaiwa kwenda kukagua Soko la Mwanjelwa bila kumpa taarifa yoyote meya wa jiji hilo. Meya alifikia uamuzi huo ndani ya ukumbi wa Mkapa muda mfupi kabla ya Makalla...

Mazito yazidi fichuka dhidi ya Anne Kilango, Baada ya Idadi ya Watumishi Hewa Shinyanga Kuongezeka Hadi 226

Rais John Magufuli ameendelea kumng’ang’ania aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango baada ya kusema idadi ya watumishi hewa katika mkoa huo imeongezeka kutoka 45 hadi 226.Aprili 11, Rais Magufuli alitengua uteuzi wa Kilango kwa kosa la kutangaza kuwa mkoa huo hauna watumishi hewa, lakini ikabainika baada ya Ikulu kufanya uchunguzi wake kuwa kulikuwa na watumishi...

Chris Brown Akiri Alitaka Kujiua Kwa Sababu ya Penzi la Rihanna

Chris Brown amesema alitaka kujiua baada ya kumshambulia aliyekuwa mpenziwe Rihanna kabla ya tuzo za Grammy mwaka 2009.Katika kipande kifupi cha makala yake ya ‘Karibu katika maisha yangu’,mwanamuziki huyo wa mtindo wa R & B amesema uhusiano wao ulikuwa kama ndoto lakini akajihisi kama hayawani.“Nilikuwa katika kilele cha dunia,nyimbo zangu zikiongoza,nikapendwa na...

Dereva Afa Maji Akijaribu Kuvuka Mto Kwa Kutumia Gari, Morogoro

Dereva tax aliyejulikana kwa majina ya Shakiru Hashimu mkazi wa Mdaula Ngerengere mkoani Morogoro amekufa maji baada ya kusombwa akiwa ndani ya gari wakati akijaribu kuvuka mto Ngerengere.Dereva huyo alikuwa akivuka mto huo ukiwa umefurika maji kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali.East Africa Radio imefika katika eneo la tukio na kukuta kikosi cha...

Rais Magufuli Atoa Somo Kwa Waandishi wa Habari..Awaomba Waitangaze Tanzania..Majirani Waache Kutangaza Maliasili za Tanzania Kuwa ni zao

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo juzi wakati wa uzinduzi wa Daraja la kisasa la Kigamboni ambalo litakua mfano Afrika mashariki, huku akiwaomba Kuandika kwa kuitangaza nchi KwanzaDkt. Magufuli amesema kuwa kama waandishi wasipoitangaza Tanzania hakuna mwingine wa kuweza kufanya hivyo na ndio maana hata nchi jirani wanadiriki kunadi maliasili za Tanzania kuwa zinapatikana...

Khari sio shwali, Lugumi...Majibu ya Jeshi la Polisi Hayarizishi..Sasa Ripoti Kutinga Bungeni

Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) haijaridhishwa na majibu yaliyotolewa na maofisa wa juu wa Jeshi la Polisi kuhusu Mkataba wa Lugumi Enterprises, na hivyo kamati hiyo imeamua kuunda kamati ndogo leo itakayochunguza kwa undani sakata hilo  ambapo ripoti  ya  uchunguzi huo itawasilishwa bungeni kama ilivyokuwa sakata la Escrow. Kwa...

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya April 21,

...

Sasa hii kiboko, Mrema..Aamua Kumfuata Magufuli Dar es Salaam ili Ampe Kazi..Adai Kuna Majipu Anayajua Akayasafishe

Mwenyekiti wa taifa wa Chama cha TLP na aliyekuwa mgombea Ubunge wa jimbo la Vunjo, Agustino Mrema anatarajia kusafiri kuja jijini Dar es salaam kwa lengo la kumpongeza Rais Magufuli na kumkumbusha ahadi aliyompa mwaka jana ya kumpatia kazi Serikalini.Akizungumza kupitia kipindi cha Sun Rise kinachoruka kupitia Times fm, Mrema amempongeza Rais kwa jitihada za ukusanyaji...

HATIMAYE Barakah Da Prince Amvisha Naj ‘Pete ya Uchumba'

Barakah Da Prince ambaye kwa sasa amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na msanii wa kike, Naj, amedai kupiga hatua zaidi kuelekea kwenye uchumba.Wamefunguka exclusively kwa Bongo5 kuhusu uhusiano wao:“Yeah ni kweli mimi na Naj tuna uhusino na hadi kwetu nimeshamtambulisha na yeye kwao najulikana na pia nimemvisha pia pete, sio ya uchumba ila ni Promise Ring,” amesema Barakah.“Ndio...

Diamond Platnumz Anunua Nyumba Mpya Dar es Salaam Maeneo ya Sala Sala...Bei Aliyonunulia Ipo Hapa

Diamond platnumz ameendelea kuonyesha yeye ni msanii wa kuigwa baada ya leo hii kununua nyumba mpya iliyopo dar es salaam maeneo ya salasala mwanzo Nyumba hiyo imemgharimu diamond zaidi milion 100 za kitanzania. Wasanii wengine wanapwa kuekeza kwenye ardhi ili kesho yake wasikose pakujificha. Hongera sana kijana diamond una umri mdogo lakini unajitambua  ...

TAZAMA VIDEO Jinsi Wenje Alivyolipuaga Ufisadi wa Wilson Kabwe Mwanza...Lakini Hakuna Hatua iliyochukuliwa...Leo Kailiza Dar Pia

Mkurugenzi  wa Jiji la Dar es Salaam aliyesimamishwa kazi Jana, Wilson Kabwe kumbe alishawahi kutuhumiwa na Ufisadi mwingine alioufanya Jijini Mwanza, Tuhuma hizo zilitolewa na Wenje aliyekuwa Mbunge wa Nyamagana kipindi cha awamu ya nne...Tazama Video hii Jinsi Wenje alivyolipua Ufisadi wa Wilson Kabwe Mwanza:...

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 20,

...

Tazama takwimu ya redio na runinga zinazocheza nyimbo nyingi Tanzania

Kampuni ya kusimania haki miliki za wasanii, Copyrights Management East Africa Limited (CMEA) Jumanne hii imetoa takwimu ambazo zinaonyesha ni redio gani na runinga nchini ambazo zinaongoza kucheza nyimbo nyingi kuliko matangazo. CMEA kupitia facebook, walipost hiyo hapo juu na kuandika: Tambua vituo ishirini bora vya runinga na redio vilivyoongoza kucheza Muziki kwa...